ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, May 4, 2023

PASTOR T APENDEKEZA DCI IWASHIRIKISHE WACHUNGAJI WA KIROHO KUMHOJI MACKENZIE

 

Mchungaji Paul Mackenzie akiwa chini ya ulinzi.

Mhubiri maarufu Pastor T ameiomba serikali kuhusisha mtumishi wa kiroho katika kumhoji mchungaji wa dhehebu potovu Paul Mackenzie kwani huenda wanakabiliana na roho ya kishetani.

Katika video inayozunguka kwenye TikTok , mchungaji huyo amesema DCI haipaswi kuchukulia kirahisi semi za Mackenzie 'mnachopigana nacho hamkijui, kitawaramba'.

 Amesema kuwa kutokana na miili hiyo mingi kufukuliwa katika msitu wa Shakahola huenda ikawa imetolewa dhabihu na mchungaji huyo tata kumaanisha kuwa madhabahu ambayo DCI inajaribu kuzima inaweza isifanye kazi kwani inahusisha mambo ya kiroho.

"Hii haikuwa inahusu imani potovu. Ilikuwa ni ushirikina. Walikuwa wanatoa sadaka za binadamu. Kiongozi wao hakuaga. Na wanasema alikuwa amepangia kufunga mwisho.

Huyu mtu haifai kuhojiwa na DCI pekee, bali anapaswa kuhojiwa na watumishi wa kiroho kwa sababu anachofanya ni cha kiroho sana.

Ni kweli amevunja sheria za nchi, unaweza kumkamata mtu huyu lakini huwezi kumkamata roho yake.

Kwa sababu roho iliyofanya kazi ndani yake haitaweza kufungwa gerezani, bado itaendelea," alisema.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.