ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, April 13, 2023

MWANAMUME AOA DADA WAWILI, AJALIWA WATOTO 14 NAO: "NINAWATOSHELEZA WOTE"

 


Mwanamume mmoja anahisi fahari kwa hatua yake ya kuwaoa wake wawili na familia hiyo inaishi kwa amani katika nyumba moja.

Wanawake hao wawili wanaoshiriki mwanamume mmoja ni dada wa tumbo moja  na wanaishi kwa amani katika nyumba moja

Mwanamume huyo amesema hapo awali alikuwa ameoa mke wake wa kwanza kwa takriban muongo mmoja kabla ya kuoa mwingine, dada ya mkewe.

Mukama Mugenimwana alipendana na kuoa dadake Juliet, Namirembe Harriet, ambaye alikuwa akiwasaidia kulea watoto wao.

Juliet alikuwa amemwomba Namirembe kuwasaidia wenzi hao kutunza watoto wao wachanga alipojifungua mtoto wake wa tano.

“Nimefurahi kuwa nao wote wawili upande ingawa safari ya kuwaoa imekuwa ngumu, lakini mimi ni mume wa kujivunia, na sina aibu kwa wake zangu.

Mke wangu wa kwanza, ambaye tumeishi naye kwa takriban miaka 20, ana watoto 10 naye mke wangu wa pili ana watoto wane.

Kwa miaka minne, Mukama kwa kawaida alikuwa akimvizia Namirembe kutokana na urembo wake.

Baadaye alimeza chambo, na Namirembe akapata ujauzito wa mwanamume huyo kutoka Uganda ambaye alisema alikuwa na matatizo na mke wake wa kwanza.

"Tulikuwa na ugomvi katika maisha yetu ya kila siku hapa nyumbani na hivyo ndivyo nilivyoishia kushikana na dadake," Mugenimwana alijitetea.

Juliet alimshinikiza Namirembe amwambie ni mimba ya nani naye akamwambia kuwa ilikuwa ya mumewe

Alikusanya virago vyake akarudi nyumbani kwa wazazi ambao aliishi nao kwa muda.

Mugenimwana alilazimika kumlipia mahari Namirembe ili awachukue dada wote wawili kama wake zake na kusamehewa na wazazi wa dada hao.

Anaishi nao kwa amani na inadaiwa ni mjamzito na vile vile anatazamia kupanua familia yake.

 "Siri ya kuwapa raha wake zako ni kugawana nao kila kitu kwa usawa katika nyumba, najaribu kuwaridhisha wake wote wawili, ninawapa kila nilichonacho, nawapenda wote wawili, nafanya hivyo ili kuepusha shida.

Sitaki vita. Sitaki hata mmoja wao ahisi kutishiwa au kutothaminiwa," alisema.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.