ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, April 11, 2023

MWANAMUME AHUKUMIWA GEREZANI KWA KUSHTUA KUKU WA JIRANI YAKE HADI KUAGA DUNIA

 

Mwanamume mmoja nchini Uchina amehukumiwa kifungo gerezani kwa makosa ya kushtua kuku wa jirani yake hadi wakaaga dunia.

Mwanamume huyo kwa jina Gu anaripotiwa kuingia kisiri katika shamba la jirani yake kabla ya kushtua maelfu ya kuku na kuwaaacha wamefariki.

Mahakama ya Hengyang iliambiwa kuwa Gu alitumia tochi kuwatishia ndege hao 1100 na kuwafanya kuuana - hii ikiwa njama yake ya kulipiza kisasi dhidi ya jirani yake

inaripotiwa kuwa mwangaza huo ulifanya kuku hao waliokuwa wamshtuka kukimbilia kwenye kona na kuuana kwa kukanyagana.

Gu alikuwa akilipiza kisasi katika mzozo wao ulioanza Aprili 2022 jirani yake alipokata miti yake bila ruhusa japo alipigwa kifungo cha miezi sita gerezani.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.