ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, April 11, 2023

AFISA WA POLISI ARUSHA KITOZA MACHOZI KWA LOJI KUMCHOMOA DEMU WAKE AKIMSHUKU KUCHITI


Polisi mjini Kisumu wanachunguza kisa ambapo afisa mmoja wa polisi alirushua vitoa machozi katika maeneo kadhaa ya burudani mkesha mjini humo usiku wa kuamkia Jumatatu

Kwa mujibu wa ripoti ya polisi, kisa hicho kilitokea mwendo wa saa tisa asubuhi, polisi huyo akimshuku mpenzi wake kutoka na mwanamume mwengine.

Kisa cha kwanza kilitokea katika hoteli moja ambapo afisa huyo alishuku kuwa mpenzi wake alikuwa amekodi chumba na mwanamume mwengine.

Baada ya ugomvi na mlinzi ambaye alimzuia kuingia hotelini humo, inaripotiwa kuwa afisa huyo wa polisi alirusha kitoza machozi hotelini humo

Polisi huyo baadaye aliondoka eneo hilo kwa kutumia pikipiki baada ya juhudi za kuingia hotelini humo kukosa kufua dafu.

Mshukiwa alielekea eneo la Nyamasaria kwenye barabara kuu ya Kisumu kuelekea Nairobi na kurusha kitoza machozi katika eneo la burudani ambako wananchi walikuwa wanaburudika.

Alivamiwa na kukamatwa na umati akitambuliwa kuwa afisa wa polisi.

Alipata majeraha mabaya na kukimbiza katika Hospitali ta Mafunzo na Rufaa ya Jaramogi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.