ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, April 26, 2023

MSHIKAJI NYOKA MAARUFU AFARIKI BAADA YA KUNG'ATWA NA NYOKA MWENYE SUMU


Mshikaji mashuhuri wa nyoka nchini Uganda ambaye pia alikuwa muuzaji wa mnyama, huyo amefariki dunia baada ya kuumwa na nyoka mwenye sumu akiwa katika mawindo.

Kulingana na mkewe, Abdallah Kalule mwenye umri wa miaka 38, aliona nyoka likiingia kwenye kichuguu karibu na nyumba yao na kama kawaida alimfuata.

Kalule aliwinda nyoka na kuwauza zaidi kwa waganga wa kienyeji kwa Ksh.5,400 sawa na (93,466.13)

Nyoka huyo alimuuma na kutoroka wakati wa misheni yake ya uwindaji, na kumwacha akipambana na sumu.

Mjomba wake Kalule ambaye ni Mariam, amesema Kama kawaida, alichukua jembe na kuanza kuchimba kichuguu kikubwa. Uchimbaji ulichukua muda na nyoka kutoonekana

John Jjingo, aliongeza kuwa japo familia yake wana historia ndefu ya kukamata na kuuza nyoka, wameamua kuachana na biashara hiyo baada ya kifo cha Kalule.

Marehemu Kalule alikuwa amekamata kwa muda mrefu nyoka ambao baadhi yao walikuwa wakubwa kuliko waliomuua.

Hatuwezi kuendelea na biashara hatari kama hii ambayo inaweza kutufanya kupoteza maisha yetu.

Tutajikita katika shughuli nyingine kama vile nyanya na mahindi,” alisema Jjingo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.