ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, April 12, 2023

KWELEAKWELEA WAHARIBU MASHAMBA YA WAKULIMA

 


TAKRIBANI heka 1,600 za mashamba ya mpunga Kata ya Kagu, Halmashauri ya Wilaya ya Geita mkoani hapa, zipo hatarini kushambuliwa na ndege aina ya kweleakwelea.

Ofisa Kilimo wa Halmashauri, Malick Athuman amesema tayari mawasiliano na Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatirifu (TPHPA) yamefanyika, ili kuwadhibiti ndege hao ambao idadi yao inaonekana kuongezeka katika eneo hilo.

Amewahakikishia wakulima kwamba changamoto hiyo itaisha, kwa uendelevu wa zao hilo la chakula na biashara.

 Pamoja na kuwathibiti kweleakwelea shambani, mamlaka itapulizia dawa kwenye mazalia yao kwa kutumia helikopta, ili kuangamiza kabisa chimbuko lao,  

Amedai kuwa kawaida ndege hawa huvutiwa na mazao mengi, ikiwemo alizeti, lakini wamegundua wanapendelea zaidi mpunga kiasi kwamba wanaweza kuhama haraka kutoka shamba moja kufuata jingine.Kuwadhibiti ni lazima kwa sababu wanafanya uharibifu mkubwa kwa kuanza kushambulia mmea wenyewe, hadi pale mpunga unapoelekea kukomaa.

Ilifahamika zaidi kwamba kweleakwelea wana uwezo wa kuharibu shamba zima kwa asilimia 100, kiasi cha mkulima kutopata hata punje ya mavuno.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.