ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, April 12, 2023

JAMAA AFUMANIWA NA MKE WA BOSI WAKE NAIVASHA.


Mwanadada huyo anasemekana kuwa alikuwa na shauku kuhusu mahusiano ya mumewe na mkwe wa bosi wake kabla ya tukio hilo ila alikosa uthibitisho kamili wa iwapo ni kweli wawili hawa walikuwa mahawara.

Mwanadada huyo anayefahamika kwa jina la Mercy anasemekana kuwasikia wawili hawa wakiwa na maongezi yaliyoashiria kuwa walikuwa wanatongozana wakati ambapo bosi  wa mumewe na mke wake walipowatembelea nyumbani.

Siku ya ujio wa boss wa Robert  anasemekana kuwa na kumbukumbu ya mazungumzo waliokuwa nayo kama ifuatavyo.

Leo ni siku ya maana katika maisha yangu. bosi wangu anastahili kuona nyumba yetu ikiwa katika hali safi. Unanisikiza kweli Mecy? Mume wangu alisema kwa hasira lakini nilikwa nimezoea jinsi alivyokuwa akizungumza,""Ndio Robert nimekusikiza. Nimemtengenezea bosi wako chakula anachokipenda na nikizuri," Nilijibu

"Kabiruni ndani ya nyumba Bwana na Bi Teddy. Habari za jioni Bi Teddy, nimefurahi kukuona,” nilimsikia mume wangu akiwaeleza wageni wetu walipofika.

Inasemekana kuwa baada ya muda kidogo Bi Teddy aliomba kuonyeshwa sehemu tofauti za nyumba ya Robert wakati ambapo Mercy alikuwa akitayarisha vinyuaji.

Katika safari ya kuonyeshwa nyumba wawili hawa wanasemekana kuchukua muda mwingi kabla ya kurejea sebuleni na hapo ndipo Mercy akaamua kuwafuata na kubaini kilichokuwa kinaendelea.

Mercy anasemekana kukosa kuingia katika chumba walimo kuwa wawili hawa kwani alichosikia ni ishara kuwa wawili hawa walikuwa na mahusiano.

Kwani leo hauna kitu kwa ajili yangu?" Bi Teddy alimuuliza Robert"Bila shaka, mpenzi wangu,” Robert alijibu na hapo nikasikia sauti ya kupeana busu.

Mercy anasema japo tukio hilo lilimthibitishia kuwa mumewe na mke wa bosi wake walikuwa na mahusiano alihitaji uthibitisho zaidi.Wageni walipoondoka Mercy anasemekana kukosa kumzomea mume wake lakini badala yake akaamua kuenda kutafuta huduma za daktari wa kienyeji Wema Kamaliza.

Siku chache baada ya Kamaliza kufanya mambo yake Robert na mke wa bosi wake wanasemekana kugandana wakifanya ngono katika Lodge huko Naivasha.

Mecry alisema kuwa alikwenda kwenye gest hiyo baada ya kupigiwa simu na mumewe na kisha kuwaeleza alichokifanya na pia kuwaeleza aliyosikia wakizungumza wakati walipowatembea katika makaazi yao.

Baada ya mazungumzo na majadiliano Mercy aliwasiliana na Kalumanzila wake  ambaye alikuja na akawatenganisha wawili hawa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.