ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 23, 2023

WEZI WAFUKUA KABURI NA KUIBA SEHEMU ZA MWILI SAA CHACHE BAADA YA MAZISHI


Watu wasiojulikana  wamefukua kaburi na kunyofoa sehemu za siri za mwili wa marehemu Ruben Kasala, aliyezikwa Machi 18, 2023.

Mtoto  wa marehemu Frank Kasala alisema baba yake Ruben Kasala alikuwa akiugua kisukari na kukumbana na matatizo ya mapafu tangu Machi 2023

Baada ya kupata habari za kifo cha baba yake asubuhi ya Machi 18, walifanya mazishi baadaye siku hiyo hiyo

 Amesema kulingana na mila na desturi zao, ni lazima warejee walikomzika baba yao asubuhi iliyofuata.Walipofika, walikuta kaburi limefukuliwa na jeneza limevunjwa.

Waligundua pia marehemu baba yao mwenye umri wa miaka 74, hakuwa na baadhi ya sehemu za mwili. Lakini baadaye walizika tena mwili huo upya.

Baadhi ya jamaa wengine wa marehemu walionyesha masikitiko yao baada ya kupata taarifa hizo na kueleza kuwa bado hawajabaini sababu kuu iliyopelekea mwili huo kufukuliwa.Walihusisha tukio hilo na imani za kishirikina na uchawi.

Wakati hayo yakijiri, kule nchini Kenya nako Jamaa afukua mwili wa shemejiye Katika tukio tofauti la kufanana na hilo,

kulikuwa na kisa cha ajabu katika kaunti ya Migori baada ya mwanamume mmoja kuufukua mwili wa shemeji yake uliozikwa katika boma lake miaka 12 iliyopita.

Isitoshe, mwanamume huyo alichukua mabaki hayo ya shemeji yake na kuweka kwenye gunia na kwenda kuyatupa kwa mke wake wa zamani Monica Adhiambo.

Ripoti ya polisi ilisema kuwa mwanamume huyo alitengana na Adhiambo mwaka wa 2020, na alifanya kitendo hicho cha ajabu kupinga kutemwa na mke wake wa zamani, ambaye dada yake Joan Apondi alikuwa amezikwa nyumbani kwake

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.