ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 23, 2023

MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU APATIKANA AMEFARIKI NYUMBANI KWAKE SIKU CHACHE BAADA YA KUGOMBANA NA MPENZIWE

 

Polisi huko Kabale wanajaribu kusuluhisha mauaji mawili yaliyounganishwa baada ya mwili wa Sarah Naturida, uliotazama chini ukiwa umefungwa mikono kupatikana katika chumba chake cha alichopanga

Babake, Naris Ndanganwa alikuwa na wasiwasi baada ya kutosikia chochote  kutoka kwa bintiye kwa siku mbili na akampigia simu mwenye nyumba wa Naturida ili kuuliza aliko.

Ni mawazo ya babake ambayo yalisababisha msako wa polisi. Msemaji wa polisi mkoani Kigezi, Elly Maate, alithibitisha hilo walipouliza kutoka kwa majirani zake na mwenye nyumba.

Maafisa wa polisi, mwenye nyumba na babake Naturida walifika chumbani kwake, wakakuta kimefungwa na kuvunja kufuli. Hapo ndipo maiti yake ilipopatikana.

Kulingana na walioshuhudia kioja hicho, mrembo huyo alizozana na Denis Arinaitwe; mwanamume anayeaminika kuwa mpenzi wake Jumapili asubuhi.

Hili liliwashangaza polisi kwa sababu Arinaitwe tayari yuko chini ya ulinzi wao  baada ya kumpiga risasi mpenzi wake, polisi mwanamke, Caroline Komugisha, katika makazi yake kambini.

Alijaribu kujitoa uhai, lakini alikamatwa na maafisa wengine wa polisi waliokuja mbio baada ya kusikia milio ya risasi. Kulingana na gazeti la Monitor, uchunguzi unaendelea ili kubaini kile ambacho kingeweza kusababisha Arinaitwe kumuua msichana huyo wa polisi

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.