ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 23, 2023

MWANAHABARI WA UFARANSA ALIYESHIKILIWA NA WANAMGAMBO NCHINI MALI KWA MIAKA SABA AREJEA NYUMBANI.

 


Mwanahabari Olivier Dubois  mwenye umri wa miaka 48 kutoka Ufaranasa Jumanne amerejea nyumbani baada ya kushikiliwa kwa karibu miaka 7 kwenye eneo  la Sahel.

Mwanahabari huyo alilakiwa na familia yake pamoja na rais Emmanuel Macron, kwenye uwanja mmoja wa ndege karibu na mji mkuu wa Paris.


Dubois akiwa na mfanyakazi wa kutoa msaada Jeffery Woodke mwenye umri wa miaka 61 kutoka Marekani walikamatwa kusini magharini mwa Niger Okotoba 2016, na waliwasili kwenye mji mkuu wa taifa hilo wa Niamey Jumatatu baada ya kuachiliwa huru.


Video iliyotolewa awali na watu waliokuwa wamemshikilia inasema kwamba walikuwa ni kutoka kundi la Support Group for Islam and Muslims, GSIM, ambalo linajumuisha makundi ya kigaidi ya Sahel, na linalohusishwa na lile la Al-Qaeda.

Dubois alikuwa akiishi nchini Mali tangu 2015 wakati akiwa mwanahabari huru wa gazeti la Ufaransa la Liberation, pale alipokamatwa. Hakuna taarifa za kina zilizotolewa kuhusu Dubois na mwenzake Woodke.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.