ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 4, 2023

WATU 18 MBARONI WAKIWEMO WAALIMU KWA TUHUMA ZA KUIBA TSH 273 KWA MTANDAO.


Jumamosi, Machi 04, 2023


Jeshi la polisi Mkoani Mwanza linawashikilia watu 18 kwa tuhuma mbalimbali wakiwemo walimu wanane wa shule za msingi wanaodaiwa kuiba zaidi ya Sh273 milioni kutoka Benki ya Walimu (MCB) kwa njia ya mtandao Mwanza.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Wilbroad Mutafungwa amewaambia waandishi jijini Mwanza ijumaa Machi 3, 2023 kuwa walimu hao wanaotoka shule tofauti wanadaiwa kufanya wizi huo Februari 20, mwaka huu kwa kujihamishia fedha kwenye akaonti zao baada ya kuingilia mawasiliano na mfumo wa benki.

Amewataja wanaoshikiliwa na shule wanazotoka kwenye mabano kuwa ni Gasper Maganga (shule ya msingi Kilabela) Wilaya ya Sengerema, Marwa Mwita (shule ya msingi Nyitundu Sengerema), Masaba Mnanka (Shule ya Msingi Kilabela), Harold Madia (Bugumbikiswa), Clever Banda (Sekondari ya Nyamatongo Sengerema), Justin Ndiege (Shule ya Msingi Ishishangolo), Fredrick Ndiege (Pamba C) na Steven Sambali anayetoka shule ya msingi Nyangongwa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.