ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 18, 2023

"UHURU NDIYE ALIFANYA RAILA KUTOCHAGULIWA" PASTA EZEKIEL ASEMA

Pasta maarufu Ezekiel Odero (kushoto) amesema Raila Odinga (kulia) alipoteza uchaguzi wa urais mwaka jana kwa kujihusisha na aliyekuwa rais Uhuru Kenyatta.


Odero alisema Wakenya hawakumtaka Uhuru na hivyo kisu chao kikapita na kumkata Raila kwa sababu alikuwa rafikiye. Amemuonya Rais William Ruto kuwa waliomshabikia na kumchagua bado watamgeuka na kumwangusha.


“Hawa hawakupendi, ni kwa sababu hawakumpenda Kenyatta na wewe ulijitenga na yeye na hivyo wakakuona kama chaguo. Lakini si eti wanakupenda, hawa watu hawakupendi,” alisema Odero. Odero ametabiri kuwa hivi karibuni Rais Ruto atapokea upinzani mkali kutoka kwa wananchi.


“Rais niskie, hawakupendi. Usipowapa kile wanataka, wembe ni ule ule,” mhubiri huyo alimwambia Rais. Alisimulia kuwa wapiga kura huwachagua viongozi ila huwa wanakataa wapinzani kwenye debe na ndipo wengine kuibuka washindi.


“Walimkataa Moi, wakamchagua Kibaki. Kisha wakamkataa Kibaki tena, 2013 walichagua Uhuruto . . . kisha wakawakataa tena. Mimi Rais Ruto nakwambia wafanyia kazi kwa moyo mmoja lakini usidhani wanakupenda,” aliongeza. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.