ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 24, 2023

SHERIA MPYA YA KUTOBADILI IMANI YA KIDINI NCHINI INDIA YALALAMIKIWA


Viongozi ya makundi ya walio wachache nchini India wanasema kwamba sheria mpya ya kutobadili Imani iliyopitishwa katika baadhi ya majimbo inalenga kuadhibu na kukandamiza makundi ya wakristo na waislamu nchini humo.

Hayo yamejiri wakati tume ya Marekani ya Uhuru wa kimataifa wa dini, USCRIF, ikieleza wasiwasi wake kutokana na sheria hiyo, na kuomba ibatilishwe.

USCRIF kupitia ripoti imesema kwamba sheria hiyo mpya inavuruga uhuru wa kidini nchini India, ambao tayari ulikuwa hatarini, na kwamba hatua hiyo ni kinyume na sheria za kimataifa za haki za binadamu.

Makundi ya kihindu pamoja na chama tawala cha Hindu Nationalist Bharatiya Janata, wanadai kwamba wamishonari wa kikristo wanabadili Imani za watu kote nchini kwa kutumia nguvu au ushawishi usiofaa.

 

Katika miaka ya karibuni, wamedai kwamba waislamu wamekuwa wakivuta watu kwenye dini yao kupitia njia haramu.

 

Kufikia sasa majimbo 12 kati ya 28 yaliopo nchini humo yamepitisha sheria hiyo, wakati baadhi ya yaliobaki yakitathimini kufuata nyayo .

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.