ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, November 4, 2022

HII HAPA HIFADHI YA TAIFA ILIYO KATIKATI YA JIJI LA MWANZA

NA ALBERT G. SENGO/MWANZA Katika kuthibitisha uzalendo wa kweli wa kuthamini na kutambua rasilimali za taifa zitonakazo na sekta ya utalii, watanzania wamehimizwa kujenga utamaduni wa kutembelea hifadhi ya taifa ya kisiwa cha saa nane, ili kuchangia pato la taifa kwa ustawi wa maendeleo. Mkuu wa hifadhi ya taifa ya kisiwa cha saanane Eva Malya, amesema hifadhi hii inavivutio mbalimbali, yakiwemo maeneo ya mapumziko, eneo maalum la usiri la kushuhudia mandhari nzuuri ya ziwa Victoria, jiwe maarufu la kuruka pamoja na ongezelo la ndege na wanyamapori. Ndani ya hifadhi hii kinachostaajabisha watalii wengi, ni jinsi tabia ya ndege dume aina ya tausi inavyojidhihiri akiwa kwenye imaya yake, Hilda Mikongoti ni afisa uhifadhi hifadhi ya taifa ya kisiwa cha saanane. Mkuu wa hifadhi ya taifa ya kisiwa cha saanane Eva Malya, amesema utakapotembelea hifadhi hii hutojutia kupoteza mudauzuri wa hifadhi hii unaelezwa na baadhi ya watalii wa ndani, waliotembelea hifadhi ya saanane.



Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.