ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, October 17, 2022

MWANAUME ALIA BAADA YA MPENZIWE KUWA NA UHUSIANO NA MTU ALIYEDAI KUWA BINAMUYE.

Mwanamume huyo alisema walitengana na mpenzi wake baada ya miaka miwili.
Picha: @kinyuaWaMuthoni. Chanzo: Twitter 

Mwanamume aliyetambulika kama Kinyua Wa Muthoni, amewasisimua wanamitandao kwenye Twitter, baada ya uhusiano wa miaka miwili na mpenzi wake kufika kikomo ghafla. 

Kwenye misururu ya jumbe za Twitter zilizoonekana mwanamume huyo aliyevunjika moyo alisema alisitisha uhusiano baada ya kugundua mpenzi wake alikuwa akimchezea akili. 

Kwa mujibu wa Kinyua, mwanamke huyo alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamume aliyemfahamu na aliyetambulishwa kwake kama binamu wa mpenzi wake mnamo Januari. 

"Leo nimesitisha uhusiano na mpenzi wangu. Amekuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamume mwingine kisiri. Tumechumbiana na msichana huyo kwa miaka miwili. Alinitambulisha kwa jamaa zake na nilikuwa nasubiria kujuana na wazazi wake, ila ninasikitika sasa," Kinyua aliandika. 

Kinyua alichukua fursa hiyo kumfurahisha mpenzi wake na "cousin" yake ndipo aweze kumkubali ila alipigwa na butwaa. Kinyua alishangaa wakati rafikiye alipomuitia kazi ya kuweka kamera za CCTV kwenye nyumba fulani eneo la Ruaka. 

Wakati alipoendelea kufanya kazi aliona gari la binamu ya mpenzi wake na kusema analijua. 

Kinyua alisema walielekezwa kwenye nyumba moja na keyateka wa jengo hilo, na alipofika mlangoni mwa nyumba ya 'cousin' ya mpenzi wake alikutana na viatu alivyokuwa amemnunulia.

 "Keateka alitunong'onezea kuwa, 'Nafikiri yuko na girlfriend yake'. Roho ilianza kuenda mbio kwa kuona viatu vilivyofanana na vile nilivyomnunulia. Nilipobisha yeye ndiye aliyefungua mlango ila alikuwa amelewa chakari kiasi kwamba hakuweza kunitambua. 

"Nilihisi ni kama nilikuwa nanyongwa, baada ya yeye kumuarifu mwanamume huyo kwamba 'babe una wageni'.

 Nilimuita kwa mutumia majina yake yote kama yalivyokuwa kwenye kitambulishoi ndipo akapata fahamu," Kinyua alisimulia. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.