ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, September 14, 2022

UHABA WA MAJI BUSWELU, NYAKATO NA KISESA MAKAMU WA RAIS ATOA AGIZO KWA WAZIRI AWESO KUKAMILISHA MRADI WA MAJI KABLA YA KRISMASI LA SIVYO...

 

NA ALBERT G. SENGO / MWANZA

Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango ameiagiza Wizara ya Maji kuhakikisha mradi wa maji Butimba unakamilika Desemba mwaka huu. Dk Mpango ametoa agizo hilo leo Jumatano, Septemba 14, 2022 wakati akiweka jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa chanzo na kituo cha tiba ya maji Butimba kilichopo jijini Mwanza.
Makamu wa Rais amesisitiza kwa kusema kuwa suala hilo siyo utani na endapo ataona mradi huo unasuasua atakuja kula Krisimasi hapa jijini Mwanza.

Mahitaji ya maji kwa sasa kwa jiji la Mwanza ni lita milioni 160 lakini uwezo wa kuzalisha maji wa chanzo cha maji Capripoint ni lita 98 tu, hivyo baada ya mradi huu kukamilika ifikapo mwezi Disemba 2022 (kama ahadi ya kuharakisha) utaongeza lita milioni 48 na kuwa suluhu ya uhakika ya tatizo la upatikanaji wa maji hadi mwaka 2040.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.