ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, July 6, 2022

POLISI NIGERIA WAANZISHA MSAKO KWA MAPADRI WALIOTEKWA.

 


Polisi nchini Nigeria wameanzisha msako kuwatafuta mapadri wawili wa kanisa katoliki waliotekwa mwishono mwa juma, katika jimbo la Edo.

Mapadri hao Udo Peter na Philemon Oboh, walitekwa na watu wenye silaha katika barabra kuu ya Benin- Auchi.

Kisa hiki kinajiri siku chache baada ya watu wenye silaha kumteka na kumuua padri mwingine Christopher Odia, karibu na mji wa Auchi.

Katika hatua nyingine mamlaka katika jimbo la Zamfara, kuko huko nchini Nigeria zimesajili vijana 9, 000, ambao wamejukumiwa kulinda jamii na kupambana na majambazi.

Mwishoni mwa mwezi uliopita gavana wa zamfara, Bello Muhammad, aliwataka raia kununua silaha ili kujilinda dhidi ya uvamizi wa makundi ya watu wenye silaha.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.