ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, July 6, 2022

NIGERIA : WASHUKIWA WA BOKO HARAM WATOWEKA BAADA YA JELA KUVAMIWA.

 


Mamlaka nchini Nigeria, zimesema washukiwa wa kundi la kijihadi la Boko Haram, wametoweka katika gereza  la Kuje, jijini Abuja, baada  ya watu wenye silaha kuvamia gereza hilo, usiku wa kuamkia leo.

Hata hivyo mamlaka nchini humo hazijasema idadi wa washukiwa waliotoweka wakati wa uvamizi huo, ambao jeshi la Nigeria limesema lilifanikiwa kuuthibiti.

Kwa miaka ya hivi karibuni makundi ya kijadi yamekuwa yakivaimia magereza nchini Nigeria, zaidi ya wafungwa 5,000 wakifakiwa kutoroka tangu mwaka 2020.

Tukio hili limejiri muda mfupi baada ya watu wenye silaha kushambulia msafara wa rais Muhammadu Buhari, kaskazini mwa taifa hilo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.