ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, July 22, 2022

AMREF WAENDESHA MAFUNZO KWA WAKUFUNZI WA MRADI WA WAWE MKOANI IRINGA

  

Mmoja ya wakufunzi kutoka Shirika la Amref Health Africa akiendelea kutoa elimu ya usimamizi na uratibu kwa wakufunzi wa vikundi vya kijamii na vya wajasiriamali kutoka vijiji 67 vya mradi wa WAWE katika kata za mradi
Mmoja ya wakufunzi kutoka Benk ya NMB akiendelea kutoa elimu ya usimamizi na uratibu kwa wakufunzi wa vikundi vya kijamii na vya wajasiriamali kutoka vijiji 67 vya mradi wa WAWE katika kata za mradi
Mmoja ya wa washiriki wa mafunzo ya usimamizi wa fedha akiendelea kupata elimu ya usimamizi na uratibu wa vikundi vya kijamii na vya wajasiriamali kutoka vijiji 67 vya mradi wa WAWE katika kata za mradi
Mmoja ya wa washiriki wa mafunzo ya usimamizi wa fedha akiendelea kupata elimu ya usimamizi na uratibu wa vikundi vya kijamii na vya wajasiriamali kutoka vijiji 67 vya mradi wa WAWE katika kata za mradi
Baadhi ya wa washiriki wa mafunzo ya usimamizi wa fedha wakiendelea kupata elimu ya usimamizi na uratibu wa vikundi vya kijamii na vya wajasiriamali kutoka vijiji 67 vya mradi wa WAWE katika kata za mradi
Mmoja ya wakufunzi kutoka Shirika la Amref Health Africa akiendelea kutoa elimu ya usimamizi na uratibu kwa wakufunzi wa vikundi vya kijamii na vya wajasiriamali kutoka vijiji 67 vya mradi wa WAWE katika kata za mradi
Baadhi ya wa washiriki wa mafunzo ya usimamizi wa fedha wakiendelea kupata elimu ya usimamizi na uratibu wa vikundi vya kijamii na vya wajasiriamali kutoka vijiji 67 vya mradi wa WAWE katika kata za mradi

Na Fredy Mgunda,Iringa.

 
Shirika la Amref Health Africa linaendelea na utekelezaji wa miradi yake miwili, iliyopo Iringa ambako ni pamoja na Mradi wa usafi wa mazingira na uwezeshaji wanawake na mradi wa Maji na Maendeleo.

 Mradi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usimamizi na uratibu vinashiriki katika ufunguzi na uendeshaji wa semina ya siku tatu kwa wakufunzi wa vikundi vya kijamii na vya wajasiriamali kutoka vijiji 67 vya mradi wa WAWE katika kata za mradi. 

Semina hii inalenga kufundisha elimu ya usimamizi wa fedha na uongozi kwenye vikundi, uundaji wa umoja wa usimamizi wa vikundi kwenye vijiji vya mradi pamoja na kuandaa mpango kazi wa usimamizi wa vikundi na utoaji taarifa kwa kila mwezi.

Mradi wa usafi wa mazingira na uwezeshaji wanawake. (WAWE- Wash and Women Empowerment)- unaotekelezwa katika jamiii zinazolima chai na kahawa katika Halmashauri ya wilaya ya Mufindi na Kilolo. Mradi huu wa mwaka mmoja unafadhiliwa na Starbucks Foundation na kutekelezwa na shirika la Amref Health Africa. 

Mradi huo unalenga kuboresha afya na ustawi wa kiuchumi wa wanawake na vijana 87,500 katika jamii zinazolima kahawa na chai katika wilaya za Kilolo na Mufindi. Utekelezaji wa mradi huu utaondoa vikwazo vya elimu, afya bora, lishe endelevu na usafi wa vyoo na maji salama

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.