ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, May 26, 2022

"TAASISI ZA FEDHA HIVI SASA ZINATUFUATA KUTUPA MIKOPO" - VIJANA MACHINGA MWANZA WAFUNGUKA.

 Umoja wa Vijana wa CCM Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza leo wamempongeza Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa juhudi mbalimbali katika kuwaletea maendeleo Watanzania.

Boniface Zephania ni Mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Nyamagana ndiye aliyeongoza jumuiko hilo ambalo pia lilihudhuriwa na vijana wafanyabiashara wadogo maarufu kama 'Wamachinga' mkoa wa Mwanza ambapo kwa upande wao wamepongeza hatua ya Serikali kuwaondoa mitaani na sasa wako kwenye maeneo rasmi, kiasi ambacho kimezivutia taasisi mbalimbali za fedha kwaajili ya kuwapatia mikopo, kisa tu wana anuani rasmi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.