ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 26, 2022

RAIS WA UKRANE ATOA MWITO WA MATAIFA KUONGEZA UZALISHAJI WA NISHATI.

 


Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy ameyatolea mwito mataifa yenye utajiri wa mafuta na gesi kuongeza uzalishaji kufidia nakisi ya usambazaji wa nishati kutoka Urusi. 


Akihutubia kwa njia ya video kwenye jukwaa la Doha linalofanyika kila mwaka kujadili changamoto za ulimwengu, Zelensky amesema ni muhimu kwa mataifa kama Qatar kuongeza usambazaji wa gesi duniani ili kupunguza bei ya nishati. 


Amesema kutokana na uharibifu unaofanywa na Urusi nchini Ukraine, taifa lake litashindwa kusafirisha nje mazao na bidhaa zake hali itakayoathiri ulimwengu mzima. Matamshi yake yanakuja wakati Urusi inaendeleza mashambulizi yake ya kijeshi nchini Ukraine na kupuuza miito ya kukomesha vita kwa njia ya mazungumzo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.