ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 26, 2022

RAIS SAMIA KUOKOA JENGO LA HALMASHAURI LILILOSIMAMA UJENZI KWA ZAIDI YA MIAKA 10

 Kamati ya Bunge ya LAAc imekagua ujenzi wa ofisi ya Utawala ya Halmashauri ya Wilaya ya Magu na kuahidi kuifikisha kiu ya wananchi wa wilaya hiyo kuona jengo lao linakamilika nazo huduma zikitolewa toka kwenye ofisi hizo.

Sambamba na kuridhishwa utekelezaji wa mradi huo, akizungumza mara baada ya ukaguzi wa mradi, Kaimu Mwenyekiti Mhe. Aloyce Akwezi (Mb) ameipongeza Halmashauri kwa jengo imara litakalowafikishia huduma wananchi kwa karibu.
Pia amewataka TAMISEMI kuhakikisha inaleta fedha zilizobaki ili kuweza kukamilisha mradi uliochukua zaidi ya miaka kumi. Wakati huo huo, Naibu Waziri (TAMISEMI) Mhe. Dkt Festo Dugange amewahakikishia kamati kuwa amepokea maelekezo ya kuleta fedha kwa mradi huo uliogharimu takribani bil 7 na utaisha kwa wakati. Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa Ndg. Ngusa Samike amepokea salamu za pongezi na kusema ushirikiano wa viongozi wa Mkoa umeweza kuleta mafanikio. Kukosekana kwa migogoro ndio kumeleta mafanikio makubwa Halmashauri ya Magu.










Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.