ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, December 30, 2019

POLISI MWANZA YAKANUSHA KUTEKWA KWA MAKADA WAWILI CHADEMA YATOA ONYO.


Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limekanusha taarifa zilizosambaa katika mitandao ya kijamii na maeneo mbalimbali zikidai kutekwa kwa wanachama wawili wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Akizungumza na Waandishi wa Habari, Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza, ACP Muliro Muliro amesema siku ya Desemba 29, Mwaka huu Majira ya 15:00 Mtaa wa Mahina Kata ya Mahina wilayani Nyamagana kulipatikana taarifa toka kwa raia wema kuwa kumeonekana watu wawili waliohisiwa kuwa siyo watu wema wakiwa karibu na Hoteli ya Paradise na kuingia nyumba jirani iliyokuwa karibu na hoteli hiyo. Kamanda Muliro, amesema baada ya kupatikana taarifa hizo jeshi la polisi lilifanya ufuatiliaji wa haraka na kufika eneo hilo na kuwakamata watu hao wawili, ambao katika mahojiano ya awali walikataa kutoa utambulisho wao kuwa wamefika maeneo hayo kufanya shughuli gani.

Aidha Muliro kazungumzia suala la ulinzi na usalama kwa mkoa wake wa Mwanza na kutoa rai na tahadhari kwa wananchi. ZAIDI FUATILIA VIDEO HAPO JUU.


Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.