ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, November 6, 2019

WAZIRI MKUU MAJALIWA NA KATIBU MKUU CCM BASHIRU ALLY WAKABIDHI NG'OMBE 5 NA SARUJI MIFUKO 100 MAULID MWANZA


"Mhe. Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Dr. Bashiru Ally alifana ziara mkoani petu na alipita ofisi za BAKWATA za mkoa zilizopo kata ya Mbugani akakuta ujenzi wa msikiti unaendelea naye akaahidi kutoa mifuko 100 ya saruji, na ndiyo ambayo nimekuja kukabidhi leo" Ni kauli ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella na kisha akaongeza ....
"Suala la pili ambalo limenileta ni kuwa Mhe. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa Majaliwa naye ameniagiza nilete ng'ombe watano kwaajili ya kitoweo cha sikukuu ya Maulid ambayo kitaifa yanafanyika hapa Mwanza, hivyo nimekuja kukabidhi naomba kuwasilisha"
 Sheikh Mkuu Mkoa wa Mwanza Hassan Kabeke akitoa neno la shukurani kwenye makabidhiano hayo yaliyofanyika viwanja vya Furahisha jijini Mwanza.
 Mifuko ya Saruji.
  Mbele ya Ma-Sheikh wa mikoa na nchi mbalimbali hususani Kenya na Uganda wameshuhudia makabidhiano hayo.
 Ng'ombe walionona.
Heri ya Maulid Mwanza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.