ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, November 6, 2019

SHIRIKA LA NDEGE LA LUFTHANSA LAFUTA SAFARI ZA NDEGE1,300 KWA SABABU YA MGOMO.

Shirika la Ndege la Ujerumani Lufthansa limefuta karibu safari 1,300 hapo kesho na Ijumaa kwa sababu ya mgomo uliopangwa na chama kinachowawakilisha wahudumu wa ndege nchini Ujerumani.

Chama cha UFO kimewataka wanachama wake kuanza mgomo wa saa 48 kuanzia leo usiku wa manane.

Ni sehemu ya mgogoro mkali na shirika kubwa kabisa la ndege Ujerumani kuhusu mishahara na hadhi ya kisheria ya chama hicho.

Lufthansa imesema leo kuwa inatengeneza mpango maalum wa safari za ndege na abiria watahitajika kuangalia taarifa kuhusu safari zao kwenye tovuti yao.

Shirika hilo limesema litaweza kuwa na safari 2,300 kati ya 3,000 zilizopangwa kesho Alhamisi na 2,400 ya zilizopangwa Ijumaa. Karibu abiria 180,000 wataathirika na kufutwa kwa safari hizo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.