ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, November 22, 2019

WAZIRI MKUU KASIMU MAJALIWA MGENI RASMI MAADHIMISHO SIKU YA UKIMWI DUNIANI KITAIFA MWANZA


Suala la maambukizi ya virusi vya HIV vinavyosababisa ugonjwa wa Ukimwi bado linaendelea kuwakosesha usingizi wataalamu wa afya kote duniani.

Kwa mujibu wa shirika la Afya Duniani (WHO) hadi sasa ugonjwa huo umewaangamiza zaidi ya watu milioni 35, hii ni taarifa mbaya kuliko zote. 

Jeh Kipi cha kujifunza toka kwa waathirika wa virusi vya Ukimwi?
Jeh Jamii inawachukulia vipi waathirika wa virusi vya Ukimwi?
Jeh Vita dhidi ya unyanyapaa bado inapiganiwa na wana jamii?
Jeh Waathirika wa VVU wanawezajie kupata haki zao za msingi?

Majibu ya maswali haya yatajibiwa kupitia wiki ya Maonyesho ya Siku ya ukimwi Duniani, yanayo taraji kuanza tarehe 25 Novemba 2019, nacho kilele kuwa Disemba Mosi 2019 viwanja vya Rock City Mall Mwanza.

John Mongella ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, hapa anafunguka zaidi. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.