ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, November 23, 2019

RC MONGELLA AIPONGEZA REA “WAHISANI WAAHIDI USHIRIKIANO ZAIDI”


Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (katikati) ameupongeza mpango wa Serikali ya Tanzania wa usambazaji nishati vijijini kupitia REA na kubainisha kwamba ni miongoni mwa mipango bora ya uwezeshaji wananchi kiuchumi barani Afrika.

Mongella alitoa pongezi hizo wakati akizungumza kwenye mkutano wa majumuisho baina ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia mbalimbali wa Maendeleo baada ya kutembelea miradi ya nishati vijijini katika mikoa ya Kanda ya Ziwa uliofanyika Novemba 22, 2019 jijini Mwanza.

Mwenyekiti wa Bodi ya REA, Julius Kalolo akabainisha kwamba wabia wa maendeleo USAID, SIDA, Benki ya Dunia, Benki ya Afrika pamoja na Nchi za Nordic wameridhishwa na jitihada zinazofanywa na Serikali kusambaza nishati vijijini na hivyo kuahidi ushirikiano zaidi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.