ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, October 22, 2019

WAZAZI WANAWASHINIKIZA WATOTO WA KIKE KUWEKA VIJITI VYA UZAZI?


Suala la ukosefu wa maadili na malezi bora kwa watoto limetajwa kuathiri mienendo ya  wanafunzi katika Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza ambapo inaelezwa kwamba baadhi ya wazazi baada ya kushindwa kuwadhibiti watoto wao sasa wanalazimika kuwapa mbinu za kushiriki ngono bila kupata mimba.

Hayo yalielezwa na Mkurugenzi wa Shirika la KIVULINI, Yassin Ally kufuatia midahalo mbalimbali ya kutoa elimu kwa jamii ili kupinga aina zote za ukatili wa kijinsia wilayani humo nayo jamii ikifunguka kile kinachoendelea.

Hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa awamu ya pili ya mpango mkakati wa kitaifa wa kupambana na ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto (MTAKUWWA) uliozinduliwa na Halmashauri ya Wilaya Misungwi kwa kushirikiana na Shirika la KIVULINI katika Kata ya Koromije, Oktoba 16, 201 na baadae kuendelea katika Kata zingine.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.