ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, October 22, 2019

WAFANYAKAZI WA UMMA WAANZISHA MGOMO ZIMBABWE.


Kuongezeka kwa hali mbaya ya kiuchumi nchini Zimbabwe kumepelekea mamia kwa maelfu ya wafanyakazi wa umma kuanzisha mgomo.

Baraza ka Apex linalojumuisha mashirikisho yote ya wafanyakazi wa umma lenye wanachama wapatao laki 3 limetoa taarifa kwa wanahabari kwamba kutokana na kutolipwa mishahara yao na ongezeko kubwa la mfumuko wa bei maafisa wa serikali wameanzisha mgomo.

Taarifa hiyo ilisema pia kwamba kumekuwepo viwango tofauti katika uongezaji wa mishahara huku katika maeneo mengi pamoja na nyongeza ya mishahara, kwa kiasi kikubwa mishahara hiyo inakuwa imepungua.

Walimu wanaofanya kazi vijijini nchini Zimbabwe walianzisha mgomo kutokana na kulipwa mishahara kidogo.

Ni karibu mwezi 1.5 hivi sasa madaktari wa nchi hio wamegoma.

Kwa mujibu wa takwimu za shirika la kimataifa la fedha (IMF), mfumuko wa bei katika nchi hio kwa mwaka ni karibu asilimia 300.

Katika taarifa ya shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na kilimo na chakula, watu milioni 5.5 nchini humo wanahitaji msaada wa chakula.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.