ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, October 22, 2019

MAELFU YA WATU WAMEKUWA WAKIMBIZI NCHINI NIGER KUTOKANA NA MAFURIKO.

Maelfu ya watu wamekuwa wakimbizi nchini Niger kutokana na mafuriko

Mafuriko yaliyoyaathiri maeneo ya kusini mashariki mwa Niger tangu mwanzoni mwa mwezi Oktoba hadi sasa yamesaabisha watu elfu 23 kukosa makazi.
Ukame wa mwaka jana ulioikumba Niger na mafuriko yaliyoyaathiri maeneo ya kusini mashariki mwa nchi hiyo umezidisha mgogoro wa kibinadamu katika nchi hiyo ambayo mara kwa mara imekuwa ikilengwa na mashambulizi ya magaidi wa Boko Haram. 


Magaidi wa Boko Haram 
Ripoti ya mwezi Septemba mwaka huu ya vyombo vya habari vya serikali ya Niger inaeleza kuwa, kuongezeka kiwango cha maji ambacho hakijawahi kushuhudiwa nchini humo katika kipindi cha miaka 50 iliyopita kumesababisha maafa makubwa katika mji mkuu Niamey. Watu 57 wameaga dunia katika mafuriko hayo. Nigeri inapatikana magharibi mwa Afrika huku asilimia 80 ardhi ya nchi hiyo ikiwa ni jangwa. Niger ilipata rasmi uhuru wake mwaka 1960 kutoka kwa mkoloni Ufaransa. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.