ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, October 23, 2019

Mahakama yataka uthibitisho wa maendeleo ya afya ya Tundu Lissu



Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam imewataka wadhamini wa aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kwenda na uthibitisho wa maendeleo ya afya yake kesi hiyo itakapotajwa tena Mahakamani hapo

Hayo yameelezwa leo baada ya Hakimu Mkazi, Thomas Simba kuuliza maendeleo ya Lissu na Mdhamini wake, Robert Katula kudai kuwa Lissu bado anaumwa

Baada ya maelezo ya mdhamini, Wakili wa Serikali, Estazia Wilson alieleza kuwa shauri hilo lilikuja kwa ajili ya kusikilizwa, hawawezi kuendelea na watamsubiri Lissu hadi afya yake itakapoimarika

Hakimu Simba aliahirisha kesi hiyo hadi Novemba 21, 2019. Lissu na wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka matano likiwamo la kuandika habari za uchochezi kinyume na sheria ya Magazeti ya mwaka 2002

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.