ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, September 9, 2019

WAZIRI MKUU WA UINGEREZA ASEMA HASHTUSHWIN NA WABUNGE KUMPINGA.

Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson amesema leo kwamba hashtushwi na jaribio la wabunge la kutaka kupinga mpango wake wa kuitoa Uingereza katika Umoja wa Ulaya bila ya makubaliano.

Kauli hiyo ya Boris ilizua mzozo bungeni baada ya kupitishwa sheria inayomtaka acheleweshe mchakato wa Brexit au atafute makubaliano mapya na Umoja wa Ulaya.

Johnson anatarajiwa kusimamisha shughuli za bunge kwa mwezi mzima kuanzia leo, baada ya pendekezo lake la kuitisha uchaguzi wa mapema kupigiwa kura ambayo huenda ikapingwa.

Brexit, mchakato wa kijiografia muhimu zaidi katika kipindi cha miongo kadhaa nchini Uingereza, bado hauna suluhisho ikiwa ni miaka mitatu tangu raia wa nchi hiyo walipopiga kura ya maoni mwaka 2016 ya kujitoa katika Umoja wa Ulaya.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.