ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, September 24, 2019

MPC YATOA PONGEZI KWA UTEUZI WA ANTHONY SANGA.


Klabu ya waandishi wa habari wa Mkoa wa Mwanza MPC inampongeza Mhandisi Anthony Sanga aliyekuwa Mkurugenzi wa MWAUWASA kwa kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli kuwa Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Maji.

Sanga amekuwa mtendaji makini kwa muda wote aliokuwa Mkurugenzi wa MWAUWASA.

Moja ya maeneo aliyoyasimamia vizuri ni mahusiano na wadau mbalimbali Mkoa wa Mwanza.

Sisi kama MPC tumekuwa na uhusiano mzuri na Sanga kwa muda wote aliokuwa Mkurugenzi hapa MWAUWASA .

MPC inamtakia kila la heri katika utendaji wake kwa nafasi yake hiyo hiyo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.