ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, September 19, 2019

BAADA YA MIAKA 50 WANAFUNZI WALIOSOMA MWANZA SEKONDARI WAREJEA NA ZAWADI YA UWANJA WA MICHEZO


KATIKA kukabiliana na upotevu wa vipaji vya mchezo wa mpira wa kikapu mkoani Mwanza, wadau mbalimbali wametakiwa kujenga viwanja vya michezo, ili kuibua, kukuza na kuendeleza vipaji hivyo kwa maslahi ya Taifa.

Ushauri huo umetolewa na mlezi wa chama cha mpira wa kikapu mkoa wa Mwanza (MRBA) Altaf Mansoor, baada ya uzinduzi wa uwanja wa mpira wa kikapu wa shule ya sekondari Mwanza, uliojengwa na wanafunzi waliohitimu katika shule hiyo yapata miaka 50 iliyopita yaani mwaka 1968.

Uwanja huo umejengwa na wahitimu hao kwa kushirikiana na Kampuni ya Moil, baada ya mkoa wa Mwanza kuyumba katika medani ya mpira wa kikapu, kufuatia timu zilizokuwa zikitamba miaka hiyo kukosa uelekeo, ili kuangalia namna ya kuzijenga.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.