ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, August 15, 2019

SUPER CUP: LIVERPOOL YAILAZA CHELSEA NA KUWA MABINGWA.

Adrian alikuwa shujaa alipozuia penalti ya Tammy Abraham


Liverpool ilishinda kombe la Super Cup kwa mara ya nne katika historia kwa kuilaza Chelsea 5-4 kwa mikwaju ya penalti baada ya sare ya 2-2 mjini Istanbul.
Kipa Adrian alizuia penalti iliopigwa na mshambuliaji wa Chelsea Tammy Abraham kuwapatia ushindi mabingwa hao wa kombe la mabingwa Ulaya.
Chelsea ilikua imechukua uongozi katika kipindi cha kwanza kupitia Olivier Giroud lakini Sadio Mane alifunga mara mbili kuipatia uongozi Liverpool.
Penalti ya Jorginho ilisababisha mikwaju ye penlati kupigwa ambapo Liverpool iliibuka washindi.
Ushindi huo unajiri miezi miwili tu baada ya Jurgen Klopp kushinda taji lake la kwanza kama mkufunzi wa Liverpool wakati alipoiongoza Reds kuishinda Tottenham katika fainali ya kombe la mabingwa (UEFA Champions League).

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.