ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, August 15, 2019

NAIBU WAZIRI MAZINGIRA - MADHARA MAKUBWA ZEBAKI INAPOTUMIKA KAMA SABUNI KUFUA DHAHABU



DALILI zinazoashiria ugonjwa wa saratani zimejitokeza miongoni mwa wachenjuaji wa dhahabu katika mgodi wa Kebaga, kata ya Kenyamanyori Halmashauri ya Mji wa Tarime mkoani Mara kutokana na matumizi makubwa ya kemikali aina ya zebaki (mercury).

Lakini cha kushangaza baadhi ya wachenjuaji wa maeneo hayo hawana hofu na hali hiyo wakisema kuwa ni sehemu ya maisha yao ingawa wataalamu wanasema ni hatari kwao.

Uchunguzi umebaini kuwa watu hao hutumia zebaki kuchenjua dhahabu kwa mikono jambo ambalo limewaathiri baadhi yao kubadilika rangi ya asili ya mwili ikiwa ni dalili mbaya.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Mussa Sima pamoja na kulizungumzia hili na kutanabaisha juhudi za Serikali ya Awamu ya 5 pamoja na mipango mikakati ya baadaye pia amefunguka juu ya kile kinachoendelea kupitia kampeni iliyo fanikiwa kwa zaidi ya asilimia 99% 'KAMPENI YA KUDHIBITI MATUMIZI YA MIFUKO YA PLASTIKI'
Fuatilia yale yaliyojiri kupitia mahojiano yake aliyoyafanya mnamo tarehe na JEMBE FM Radio Mwanza katika ziara yake Kanda ya Ziwa..

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.