ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, August 1, 2019

POLISI MWANZA YANASA MTANDAO WA WIZI WA BODABODA

KUFUATIA kuongezeka kwa vitendo vya unyang'anyi wa pikipiki na baadhi ya vijana kujeruhiwa na hata wengine kufariki dunia, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza linawashikilia watu 18 wanaotuhumiwa kujihusisha na matukio hayo ya wizi na uporaji.
Mbali na kukamatwa kwa watu hao, polisi pia limekamata pikipiki 16 zilizokuwa zikitumika katika wizi huo.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Jumatano Julai 31, 2019 Kamanda wa polisi mkoani Mwanza, Jumanne Muliro amesema matukio hayo yametokea kati ya Januari hadi Desemba 2018,  na Januari hadi Julai, 2019.
Aliyataja maeneo yaliyoathirika ni Nyakabungo,  Nyakato,  Buhongwa, Isamilo,  Ibanda,  Kiseke,  Kishiri,  Maduka tisa,  Nyamhongoro,  Ngudu wilaya ya Kwimba na Sengerema.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.