



Akiongea wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo yanayoendelea katika Chuo Kikuu cha MUHAS, Meneja wa masuala Endelevu wa TBL ,Irene Mutingazi,alisema kuwa TBL imejitosa katika kusaidia katika sekta ya afya kama ambavyo imekuwa ikisaidia kukabiliana na huduma changamoto mbalimbali za kijamii kupitia sera yake ya kusaidia huduma za kijamii inayolenga kuwaleta Watu Pamoja Katika Ulimwengu Maridhawa. “Mafunzo haya kwa wauguzi kutoka hospitali za Dar es Salaam tuna imani yatasaidia kupunguza changamoto ya elimu ya lishe duni na ugonjwa wa Selimundo kwa kuwa wataifikisha kwa walengwa wanaowahudumia hususani akina mama wajawazito na wagonjwa wa Seli mundu”,alisema.
Aliongeza kuwa TBL kupitis sera yake ya kuifanya Dunia Maridhawa itasaidia kushirikiana na wadau mbalimbali kukabiliana na changamoto mbalimbali katika jamii hususani katika sekta ya elimu na afya.
Kwa upande wake, Rais wa Chama cha Madaktari Tanzaia,Dkt Elisha Osat,alisema sekta ya afya inakabiliwa na changamoto mbalimbali na aliwashukuru wadau kama TBL ambao wamekuwa wakijitoa kusaidia kukabiliana na changamoto mbalimbali zilizopo katika sekta hiyo. --
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.