ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, July 12, 2019

"SINGIDA MASHARIKI HAIKUWA NA MWAKILISHI MWAKA WA 9 SASA" - AFUNGUKA DC ANAYEWANIA KITI CHA LISSU.



 "Ukiangalia Jimbo hili limeishi bila mwakilishi mzuri tangu mwaka 2010, Leo hii tunavyoongea maendeleo ya jimbo la Singida Mashariki yamekuwa duni sana, kwa maana mwakilishi hakuwahi kupata nafasi hata siku moja kuongelea mahitaji ya Jimbo lake zaidi ya kushughulika na masuala ya kitaifa"

"Wananchi walitegemea mwakilishi wao angezibeba shida zao na kuzipeleka Bungeni kuiomba Serikali kusaidia kuondosha changamoto za nyanja mbalimbali, lakini hatimaye Jimbo lime kosa mwakilishi takribani mwaka wa 9 sasa"

Ni maneno ya Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Miraji Mtaturu ambaye siku ya Jumatano July 10 mwaka huu 2019 amepitishwa na mkutano mkuu wa CCM wa Wilaya hiyo kuwania ubunge wa Singida Mashariki, na hapo alikuwa akijibu ya baadhi ya maswali ya  Albert G. Sengo, mtangazaji wa kipindi cha KAZI NA NGOMA cha Redio Jembe Fm Mwanza, 

Mtaturu alipata kura 396 akifuatiwa na Mugoto Kitima aliyepata kura 79 huku mkuu wa Mkoa wa zamani wa Songwe, Chiku Galawa akipata kura 40. Kura 600 zilipigwa na hakuna hata kura moja iliyoharibika.

BOFYA PLAY kusikia hoja nyingine.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.