ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, May 5, 2019

SAA ZAHESABIKA MILANGO YA SOKO LA MADINI MWANZA KUFUNGULIWA


JUMATANO ya Tarehe 8 Mei 2019 Uzinduzi wa soko la madini kwa mkoa wa Mwanza unafanyika rasmi.

Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa ikiongozwa na Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella Jumamosi ya tarehe 04 mwezi Mei 2019 imezuru katika eneo hili maarufu la kibiashara na lenye biashara mbalimbali, Rock City Mall jijini hapa kujiridhisha na kukagua mazingira ya mahala palipotengwa kwaajili ya soko hilo.

Licha ya soko hilo kutumika kama nyenzo ya kukuza uchumi wa taifa pia linatarajiwa kufungua fursa za kiuchumi kwa mkoa, likihusisha wadau wote walio kwenye mnyororo wa biashara ya madini wakiwemo Wanunuzi, Wauzaji, TRA, Tume ya Madini, Benki na Mamlaka ya Serikali za mitaa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.