ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, April 25, 2019

SERA YA JPM 'SERIKALI YA VIWANDA' INAKWAMISHWA NA BAADHI YA WATAALAMU' MWEKEZAJI SENGEREMA AFICHUA.



TANGU aingie madarakani, tumemuona Rais John Magufuli akiwa na dhamira ya dhati ya kuanzisha viwanda ili kukuza uchumi wa nchi yetu, akisisitiza kuwa Tanzania ni kati ya nchi tajiri na kwamba hakuna sababu ya watu wake kuwa maskini.

Ni kutokana na dhamira yake hiyo, tumeona mambo kadhaa ambayo yanashabihiana na azma yake ya kuiwezesha Tanzania kuwa nchi ya viwanda yakifanyika kwa haraka na kwa ustadi mkubwa.

Kwanza, Rais ameimarisha miundombinu zikiwemo barabara,usafiri wa anga na sasa reli.

Pili ameimarisha kasi ya ukusanyaji wa mapato ya nchi, ambayo kwa sasa serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania inakusanya karibu trillioni moja kwa mwezi kutoka makusanyo ya awali ya Sh bilioni 900 kwa mwezi.

Hili ni jambo jema, maana kama Taifa hatuwezi kuanza safari ya viwanda, kama hatuna uwezo wa kukusanya kodi kutoka hasa kwa wafanyabiashara wakubwa watakaokuwa kuja kuwekeza, katika hilo kama hatayumbishwa, Rais ameliweza na naamini hawezi kuwekwa mfukoni!

Lakini pamoja na juhudi zote hizo za Mheshimiwa Rais magufuli sanjari na nguvu za Mawaziri wake,  Je wataalamu wetu wameshiriki kikamilifu kuisaka serikali ya Viwanda?

Si ndiyo hawa hawa ambao baadhi yao kila kukicha wamekuwa wakilalamikiwa huku wengine wakitumbuliwa kwa ubadhirifu, urasimu na kuchelewesha miradi?

Katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella anadhuru wilayani Sengerema ambako anashuhudia mradi mkubwa samaki, ambapo mwekezaji wake mara baada ya kafanya utafiti kutoka nchini China juu ya ufugaji samaki, anafanya uwekezaji, lakini mwekezaji huyo anakutana na zungusha zungusha za mmoja wa wataalamu nazo zinamkatisha tamaa….....

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.