ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 8, 2019

HIVI .... KIBONDE ALIKUWA KATIKA HALI GANI KWENYE MSIBA WA RUGE?



WANANCHI mkoa wa Mwanza wamekuwa watu wa awali kuuaga mwili wa aliyekuwa  mtangazaji maarufu nchini Tanzania, mshereheshaji wa dhifa mbalimbali Ephraim Kibonde aliyefariki dunia jana wakati akipatiwa huduma za matibabu katika hospitali ya Rufaa ya Bugando kabla ya mwili wake kusafirishwa kwenda jijini Dar es salaam kwaajili ya taratibu nyingine za mazishi.

Kibonde amefariki dunia alfajiri ya siku ya Alhamisi ya tarehe 7 mwezi Machi 2019 katika hospitali ya Rufaa ya Bugando, baada ya kuzidiwa ghafla akiwa mjini Bukoba ambako alikwenda kuhudhuria mazishi ya Ruge Mutahaba, na kusafiri hadi mkoani Mwanza ili kupatiwa matibabu zaidi lakini baadaye umauti ukamkuta.

Akiwa mjini Bukoba kwenye mazishi ya Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji Clouds Media  naye akiongoza kama Mc, hakuna aliyedhani kuwa saa 48 mara baada ya tukio hilo naye angetoweka.

Jeh kuna chochote ambacho kwa jicho la kibinadamu kuna yeyote angeweza kubaini? Mbunge wa Jimbo la Nyamagana Stanslaus Mabula anasimulia ya kwake aliyoyaona.......

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.