ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, November 24, 2018

WAZIRI MWAKYEMBE AITAKA SIDO KUONYESHA WELEDI KWA KUSAIDIA WAJASIRIAMALI.


 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe (katikati) akilitaka shirika la SIDO kuwasaidia wajasiriamali wa mkoa wa Tabora kutengeneza mashine za kisasa zitakazowasaidia kukausha bidhaa zao za chakula kisasa na kuziongezea thamani alipokuwa akifunga Jukwaa la Fursa za  Biashara na Uwekezaji  ambalo limefanyika  mkoani hapo kwa siku tatu leo,kulia ni Waziri wa Viwanda  Biashara na Uwekezaji Mhe.Joseph Kakunda na Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe.Aggrey Mwanri.
 Waziri wa Viwanda  Biashara na Uwekezaji Mhe.Joseph Kakunda (kulia) akizitaka taasisi zilizipo chini ya wizara yake kujipanga kukutana na uongozi wa mkoa wa Tabora kwa ajili ya kushauriana namna ya kufanikisha maadhimio ya Jukwaa la Fursa za Biashara na Uwekezaji  leo wakati kufunga jukwaa hilo mkoani hapo,kushoto ni  Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe.
 Mbunge wa Jimbo la Urambo Mhe.Magreth Sitta akitoa shukrani kwa uongozi wa Mkoa wa Tabora kwa niaba ya wabunge wenzake kufanikisha  Jukwaa la Fursa za Biashara na Uwekezaji  wakati wa ufungaji wa Jukwaa hilo liloendeshwa mkoani hapo kwa siku tatu.
 Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tabora Hassan Wakasuvi akiiomba serikali  kutafuta Mwekezaji atakaye  uendeleza na kuuboresha uwanja wa Michezo wa Ali Hassan Mwinyi uliyopo Tabora Mjini na kuwasaidia leo wakati wa kufungwa kwa Jukwaa la Fursa za Biashara na Uwekezaji mkoa hapo.
 Kaimu Mhariri Mtendaji Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN)  Bibi.Tuma Abbdalah akipongeza mwitiko wa wakazi wa Tabora katika kushiriki Jukwaa la fursa za Biasharana Uwekezaji  na hamasa ya maendeleo waliyoonyesha wakati wa kufungwa kwake leo mkoa hapo.
Mkuu wa Mkoa waTabora Mhe.Aggrey Mwanri akimweleza Mwenyekiti wa Jukwaa la Fursa za Biashara na Uwekezaji namna Mkoa huo umejipanga kuleta mabadiliko baada ya kumalizika kwa Jukwaa hilo mkoani  leo wakati wa kufungaji   Jukwaa hilo.



Na Anitha Jonas – WHUSM
24/11/2018
TABORA
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Harrison Mwakyembe ameitaka taasisi ya SIDO nchini kuonyesha weledi wake kwa kuwa tengenezea  wajasiriamali wa Mkoa wa Tabora kifaa chenye Teknolojia rahisi ya kukaushia bidhaa zao za chakula ili kuziongezea ubora.

Mheshimiwa Mwakyembe ameyasema hayo leo Mkoani Tabora alipokuwa   akifunga Jukwaa la Fursa za Biashara na Uwekezaji lililokuwa likifanyika Mkoani hapo kwa siku tatu  kwa lengo la kutangaza fursa za biashara na uwekezaji za mkoa huo pamoja na kuwajengea uwezo wajasiriamali  wa kuboresha bidhaa zao pamoja na kuona umuhimu wa rasimisha bidhaa hizo kwa ajili ya kuongeza wigo wa biashara na kipato.

“Naupongeza uongozi wa Mkoa huu kwa hatua waliyochukua kufikia maadhimio ya kugawana majukumu ya kuendeleza sekta  ya viwanda kimkakati  kwa kuhakikisha kila wilaya inawajibika kuleta maendeleo kwa wananchi wake pamoja na Halmashauri ya Mji wa Tabora kutekeleza utengaji wa eneo la uwekezaji  kwa ajili ya maendeleo ya viwanda hakika jukwaa hili limesaidia kutia chachu ya mafanikio katika mkoa huu,”alisema Mhe.Mwakyembe.

Naye Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji Mhe.Joseph Kakunda aliwasihii waandaaji wa Jukwaa hilo ambao ni Kampuni ya Magazeti Tanzania (TSN) kuhakikisha wanatembelea Mikoa yote nchini na baada ya hapo kushuka katika ngazi ya Wilaya kama alivyoagiza Mhe.Waziri Mkuu Kassim Majiliwa katika ufunguzi wa Jukwaa hilo.

“Kwa kuzingatia manufaa ya Jukwaa hili nimeziagiza  taasisi zilizopo chini ya Wizara yangu kujipanga na kuja hapa Tabora na kuzungumza na  viongozi wa Mkoa huu pamoja na kutoa ushauri wa kitaalamu ili kufanikisha maadhimio ya Jukwaa hili kwa manufaa ya taifa,”alisema Mhe.Kakunda.

Kwa upande Kaimu Mhariri Mtendaji (TSN) Bibi.Tuma Abdallah aliupongeza uongozi wa Mkoa huo pamoja na kuwashukuru Mawaziri waliyoshiriki Jukwaa hilo kwa uwepo kwani uwepo wao umesaidia kufanikisha jukwaa hilo na kulifanya kuwa la kihistoria kwa mikakati iliyowekwa ili kufanikisha utekelezaji wa maadhimio yake.

“Katika Jukwaa hili la nane  tangu tumeanza  uendeshwaji wa Jukwaa hili nimejifunza kuwa Tabora ina hari ya hali ya juu ya kupata maendeleo kwa namna walivyojikita katika mijadala na hoja mbalimbali wanazo ziibua hii yote inaonyesha kiu kubwa ya wananchi wa Mkoa huu kutaka kupata maendeleo”alisema Bibi.Tuma.

Pamoja na hayo nae Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe.Aggrey Mwanri alisisitiza kuwa uongozi wa mkoa hautakubali  ujio wa Jukwaa hilo kutowaletea manufaa kwani kwa maadhimio ya jukwaa hilo  wamejipanga vizuri kuhakikisha  kila Wilaya inatekeza mradi ambao utaleta manufaa kwa wananchi wake kwa kutelekeza  hilo Wilaya ya Urambo itajenga  Kiwanda cha Tumbaku,Wilaya ya Kaliua itaandaa ranchi pamoja  kiwanda cha alizeti na karanga halikadhalika uuzaji wa mazao ya misitu kwa kuzingatia sheria,Wilaya ya Uyui itasimamia masoko ya Kilimo na Mifugo na Wilaya ya Nzega kuanzisha Kiwanda cha uchakataji wa Nyama na Ngozi pamoja na kuanzisha ranchi pamoja na Wilaya ya Igunga kutekeleza kilimo cha Mpunga.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.