ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, November 23, 2018

MWAKYEMBE HATOWAACHA WALIOPUUZA USHIRIKA WA JUKWAA LA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI


 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akisisitiza umuhimu wa viongozi wa Juu katika Taasisi za Viwanda na Biashara kushiriki Jukwaa la Fursa za Biashara na Uwekezaji linaloendelea Mkoani Tabora leo wakati wa kikao cha uwasilishwaji wa mada,wa kwanza kulia ni Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji Mhe.Joseph Kakunda na wakwanza kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya TSN Bw.Habbi Mkwizu.
 Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji Mhe.Joseph Kakunda akitoa maelekezo ya kila mkoa kutenga eneo la uwekezaji ambalo litawekewa miundombinu yote muhimu kama Maji,Umeme,Barabara na Huduma za kijamii ili kuweka mazingira rafiki ya kuvutia wawekezaji,leo wakati wa uwasilishaji mada katika Jukwaa la Fursa za Biashara na Viwanda leo linaloendea Mkoani Tabora.
 Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akisisitiza suala la Wakurugenzi wa Halmashauri kusaini makubaliano na ofisi yake mara baada ya hitimisho la Jukwaa la Fursa za Biashara na Uwekezaji linaloendelea Mkoani Tabora leo katika kikao cha uwasilishwaji wa madambalimbali.
 Mkurugenzi Mkuu wa Export Processing Zones Authority (EPZA) Kanali Mstaafu Joseph Simbakalia akionyesha Jezi ya Michezo inayotengenezwa hapa nchini na kuuzwa nje ya nchi na moja ya Kiwanda kilichopo Morogoro kinachosimamiwa na EPZA ambapo alipokuwa akiwasilisha mada ya namna ya kuvutia wawekezaji nchini kutoka nje katika Jukwaa la Fursa za Biashara na Uwekezaji linaloendelea Mkoani Tabora leo.
 Mkuu wa Wilaya ya Uyui Mkoani Tabora Mhe.Gift Msuya akichangia mada wakati wa uwasilishaji wa mada mbalimbali uliyokuwa ukifanyika leo katika Jukwaa la Fursa za Biashara na Uwekezaji  linaloendelea Mkoani Tabora.
Mkurugenzi Mkuu wa Export Processing Zones Authority (EPZA) Kanali Mstaafu Joseph Simbakalia akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Tabora andiko la EPZA linaloonyesha namna ya kujenga mazingira uwekezaji bora na kutafuta masoko ya kimataifa kwa bidhaa utakazozalisha leo katika Jukwaa la Fursa za Biashara na Uwekezaji  linaloendelea Mkoani Tabora.



Na Anitha  Jonas – WHUSM
23/11/2018
Tabora.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt. Harrison Mwakyembe amewataka watendaji wakuu wa taasisi zinazohusika na Uwekezaji na Biashara nchini kutopuuzia ushiriki akatika Jukwaa la Fursa za Biashara na Uwekezaji inaloratibiwa na Kampuni ya Magazeti  Serikali (TSN).

Mheshimiwa  Mwakyembe ametoa tamko hilo leo Mjini Tabora alipokuwa  akiendesha mijadala inayotokana na uwasilishwaji wa maandiko mbalimbali yaliyokuwa yakiwasilishwa katika Jukwaa la Fursa za Biashara na Uwekezaji linaloratibiwa na TSN na kusisitiza kuwa kwa viongozi wa taasisi ambazo zimepuuzia ushiriki  nitatoa yao taarifa kwa Waziri Mkuu.

“Watendaji  wakuu wa Taasisi za Uwekezaji  hili Jukwaa siyo la kulichukulia mzaha kwa sasa tunataka kujenga nchi ya Viwanda na kuboresha mazingira yetu ya uwekezaji nyinyi ndiyo wakutoa taarifa rasmi kwa  watanzania na wajasiriamali wengi nchini hawana uwelewa mzuri wa kuendesha shughuli zao kisasa na utaratibu wa kurasimisha biashara zao, hivyo ili tupige hatua ni lazma tuboreshe mazingira ya ndani ya nchi yetu kwa kuwaeleza wajasiriamali wetu fursa zilizopo na namna ya kuzifikia,” alisema Dkt.Mwakyembe.

Akiendelea kuzungumza katika Jukwaa hilo Waziri Mwakyembe aliuagiza uongozi  wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) kuanzia Jukwaa  lijalo litakalo andaliwa na TSN nao kushiriki kikamilifu bega kwa bega ili kuongeza tija katika kufanikisha azma ya nchi kufikia uchumi wa Viwanda na Uchumi wa Kati kwa kutangaza fursa za uwekezaji zilizopo  Mikoani ili kuvutia wawekezaji  mbalimbali.

Naye Waziri wa Biashara Viwanda na Uwekezaji Mhe.Joseph Kakunda  alisisitiza kuwa kwa Taasisi ya SIDO na TBS Wakurugenzi wake kushindwa kufika ua kuelekeza kiongozi yoyote wa juu kumwakilisha na badala yake kumpa Afisa wa ngazi ya chini basi ni lazma atawajibika kujieleza kwa barua kwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo kwa kushindwa kutekeleza majukumu yake.

“Sasa ifike mahali tuache masihara katika masuala ya kujenga taifa  katika Jukwaa hili tumeona Watendaji wa Wakuu mbalimbali wa Taasisi wamewasilisha maandiko yao na kueleza mipango madhubuti wanayotekeleza na fursa zilizopo na ni utaratibu gani unaweza kutumika kufanikisha mazingira mazuri ya biashara na ukuaji wa viwanda,” Mhe.Kakunda.

Pamoja na hayo Mhe.Kakunda amewataka Wakuu wote wa Mikoa  kujipanga na kutenga maeneo ya uwekezaji ambayo yatahakikishwa yanawekewa miundo mbinu  yote muhimu  kama Maji,Umeme,Barabara na Huduma za kijamii ambazo zitasaidia kuvutia wawekezaji.

Hata hivyo Waziri huyo wa Viwanda Biashara na Uwekezaji aliendelea kusisitiza kuwa kwa viwanda vilivyokuwa vimepewa wawekezaji na wawekezaji hao kushindwa kuviendeleza serikali haitakubali viwanda hivyo kuwa magofu bali itavichukua na kutafuta wawekezaji wengine watakao viendeleza.

Halikadhalika nae Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe.Aggrey Mwanri  alisisitiza kuwa kwa upande wa Wakurugenzi wa Halmashauri Mkoa huo mara baada ya kufungwa kwa Jukwaa hilo watasaini makubaliano katika yao na Mkuu wa Mkoa ya namna wataenda  kutekeleza miradi mitatu kwa halmashauri zao kufuatia elimu waliyoipata katika jukwaa hilo na kwa Mkurugenzi atakayeshindwa kutekeleza hilo hatosita kumchukulia hatua kali sababu hatoshi kwa Mkoa wa Tabora unaoangazia maendeleo na ukuaji wa uchumi kwa sasa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.