Skip to main content

MAADHIMISHO YA WIKI YA ZIMAMOTO NA UOKOAJI KITAIFA YAFUNGWA JIJINI DODOMA.


Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, CGF Thobias Andengenye, akitoa taarifa ya Maadhimisho ya Wiki ya Zimamoto na Uokoaji Kitaifa, wakati wa kufunga maadhimisho hayo yaliyofanyika katika Uwanja wa Jamhuri uliopo Jijini Dodoma jana.
Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Kitengo cha Maokozi toka Makao Makuu wakimuonesha Kamishna Jenerali wa Jeshi la Uhamiaji Dkt. Anna Makakala, jinsi wanavyoweza kufanya maokozi kwenye majengo marefu pindi ajali inapotokea, alipotembela Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma wakati wa kufunga maadhimisho ya Wiki ya Zimamoto na Uokoaji Kitaifa yaliyoanza Agosti 29, 2018 Jijini humo jana.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Uhamiaji Dkt. Anna Makakala, akipokea zawadi ya kizimia moto cha awali (Fire Extinguisher) kutoka kwa Mkaguzi Msaidizi wa Zimamoto Philibert Chaki, alipotembelea banda la Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wakati wa kufunga maadhimisho ya Wiki ya Zimamoto na Uokoaji Kitaifa yaliyoanza Agosti 29, 2018 Jijini Dodoma jana.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamto na Uokoaji, CGF Thobias Andengenye akimkabidhi cheti mwakilishi wa TCRA, ambaye jina lake halikupatikana kwa mchango wake wa kufanikisha Maadhimisho ya Wiki ya Zimamoto na Uokoaji Kitaifa, wakati wa kufunga maadhimisho hayo yaliyoanza Agosti 29, 2018 katika Uwanja wa Jamhuri uliopo Jijini Dodoma jana.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamto na Uokoaji, CGF Thobias Andengenye akimkabidhi zawadi ya kikombe Konstebo wa Timu ya Polisi Dodoma, Ally Juma mara baada ya kufanikiwa kupata ushindi wa bao moja dhidi ya wapinzani wao Timu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, mechi iliyochezwa katika Uwanja wa Jamhuri, wakati wa kufunga maadhimisho ya Wiki ya Zimamoto na Uokoaji Kitaifa yaliyoanza Agosti 29, 2018 Jijini Dodoma jana.
Msanii Mrisho Mpoto na kundi lake wakitumbuiza wimbo maalum wenye maudhui ya Wiki ya Zimamoto na Uokoaji, mbele ya Mgeni rasmi Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamto na Uokoaji, CGF Thobias Andengenye, wakati wa kufunga maadhimisho ya Wiki ya Zimamoto na Uokoaji Kitaifa yaliyoanza Agosti 29, 2018 katika Uwanja wa Jamhuri uliopo Jijini Dodoma jana. (Picha zote na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji)

Maadhimisho ya Wiki ya Zimamoto na Uokoaji Kitaifa yalizinduliwa rasmi na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Kangi Lugola (Mb) Agosti 29, 2018 katika Uwanja cha Jamhuri Jijini Doodma na kufungwa jana Agosti 31, 2018 na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, CGF Thobias Andengenye. Kauli mbiu ya Maadhimisho ya Wiki ya Zimamoto na Uokoaji Kitaifa mwaka huu ni “SHIRIKI KUKUZA UCHUMI WA VIWANDA KWA KUFUNGA VING’AMUAMOTO VIWANDANI”

Comments

Popular posts from this blog

MAPINDUZI MAKUBWA UCHAGUZI WA MZFA YAFANYIKA MWENYEKITI APETA, KADUTU AUKWAA UWAKILISHI VILABU KWA ASILIMIA 100

Na ALBERT G. SENGO MWANZA MWENYEKITI wa Chama cha Mpira wa miguu Mkoa wa Mwanza(MZFA) Jackson Songora ametetea nafasi yake kwa miaka mingine   minne baada ya kuchaguliwa tena na wajumbe wapatao 17 kati ya 30 wa mkutano mkuu wa chama hicho Mkoani humo. Uchanguzi huo umefanyika jana katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza ambapo awali wagombea mbalimbali walijinadi kwa   wajumbe wa mkutano huo ili kuwashawishi kuweza kuwachagua katika nafasi walizomba ikiwemo ile ya Mwenyekiti, Makamu mwenyekiti, Katibu, Katibu msaidizi, Mweka Hazina na Mjumbe wa mkutano mkuu wa TFF, Mjumbe mwakilishi wa Vilabu na Mjumbe wa kamati ya udendaji.   Akitangaza matokeo hayo Mwenyekiti wa Kamati ya uchaguzi huo Richard Mgabo (pichani aliyesimama) nafasi ya Mwenyekiti iliyokuwa na wagombea wawili ambapo   Jumbe Maghati na Jackison Songora walichuana vikali.. Hapa mwenyekiti wa uchaguzi huo anaweka mambo hadhalani..... Bofya play. Ikafuata nafasi ya Katibu mkuu ...

MBUNGE WA ILEMELA ABAINISHA UBABAISHAJI MKUBWA ULIOFANYWA UJENZI WA BARABARA MPYA YA BUZURUGA, PASIANSI, SANGA, KILOLELI.

  Mbunge wa wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza Highness Kiwia (wa kwanza kulia) akijionea uharibifu kwenye mitaro ya barabara  mpya iliyo katika zama zake za mwisho kuelekea kukabidhiwa kwa halmashauri, kupitia mvua iliyonyesha kwa muda mfupi tu hapa jijini kiasi cha mifereji hiyo kumomonyoka kama biskuti kuashiria ujenzi wa kiwango cha chini uliofanywa na mkandarasi husika. Aliyenyoosha kidole ni mbunge wa Ukerewe Salvatory Machemli aliyeambatana naye. Msikilize hapa chini.... Ni barabara ya Kilimahewa, Buzuruga, Pasiansi, Sanga, Kiloleli  nayo kabla ya kukabidhiwa dosari kubwa zimeanza kujitokeza. Ziara hii imekuja wakati kikao cha Bodi ya Barabara Mkoani Mwanza kilipokuwa kimeketi na kukaa na wadau wa Wizara ya Ujenzi pamoja na wakala wa ujenzi wa barabara mbalimbali mkoani Mwanza na kikao hicho kukwepa shauri la Mbunge wa ilemela la kuishauri kamati hiyo kufanya upya uthamini wa barabara hiyo kabla ya kukabidhiwa halmashauri. Kutitia kwa tabaka la ...

DRINKINGS SUPPLY FOR CEREMONIES AND SPECIAL FUNCTION