ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, September 25, 2018

ELIMU YA MASAFA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI.

 Dkt. Peter Kilima kutoka Mradi wa Kuimarisha Mifumo ya Sekta za umma PS3, akitoa maelezo kuhusu mafunzo ya Elimu kwa Masafa kwa Madiwani.
 Dkt. Adephonce Fuka, kutoka Chuo kikuu Huria akitoa mada kuhusu mwenendo wa Elimu ya Masafa kwa Madiwani katika Mkutano wa 34 wa Jumuiya ya Serikali za Mitaa ALAT jijini Dodoma.


 Baadhi ya Madiwani wakiwa katika Mkutano huo wa 34 wa Jumuiya ya ALAT, huku wakitazama na kuona jinsi watakavyokuwa wakinufaika na Elimu ya Masafa kupitia Simu zao za Adroidi. (Picha na Habari na Atley Kuni wa OR TAMISEMI)


Elimu ya Msafa kuwajengea uwezo MadiwaniNa. Atley Kuni- OR TAMISEMIMadiwani kote nchini wataanza kupata mafunzo ya uongozi kwanjia   ya   masafa   kupitia   mtandao   wa   kielektroniki,   yaani   kupitiamfumo   wa   intaneti,   hali   itakayowawezesha   kujiimarisha   katikautendaji wa majukumu yao ya kila siku na kuwatumikia wananchi.

Akitoa mada katika mkutano mkuu wa 34 wa Jumuiya ya Serikaliza   Mitaa   nchini,   Mhadhiri   wa   chuo   Chuo   Kikuu   Huria,   Dkt.Adephonce   Fuka,   alisema   shabaha   ya   mafunzo   hayo   nikuwajengea uwezo Madiwani ambao ni wawakilishi wa wananchikatika maeneo yao.

 Akizungumza wakati wa mawasilisho, Dkt. Fuka alisema nia kuu nikuhakikisha Madiwani  wanatekeleza  majukumu   yao   kwa mujibuwa   sheria,   taratibu   na   kanuni   zinazoongoza   mabaraza   yamadiwani, na mafunzo hayo ni maboresho ya kitabu cha rejea yaMh.   Diwani   kilichotumika   kufundisha   Madiwani   kutoka  Mamlakaza Serikali za Mitaa 93 hapo awali.

Mafunzo   hayo   ambayo   yameandaliwa   kwa   mtindo   wa   Elimu-Masafa ili kuwezesha kujifunza mahali popote, yataendeshwa naChuo cha Serikali za Mitaa - Hombolo, na  ni marejeo ya mafunzoya awali ambayo yalitolewa kwa viongozi hao kwa Halmasahuri 93zilizopo chini ya mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma(PS3).

Akitoa maelezo ya awali kabla ya kutolewa kwa wasilisho la elimuhiyo ya masafa kwa njia ya kieletroniki, mwakilishi kutoka PS3,Dkt. Peter Kilima, alisema mradi huo unaofadhiliwa na Serikali yaMarekani kupitia Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani(USAID),   unafanya   kazi  katika  mikoa   13   na   Halmashauri   93   natayari umejipanga kutoa elimu kwa madiwani nchi nzima.

“Mradi   huu   ni   wa   miaka   mitano,   na   moja   ya   maeneotunayoimarisha ni mfumo ya Utawala Bora na Ushirikishwaji wa Mfumo wa Kielektroniki.



Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.