ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, August 6, 2018

WANAWAKE WATATU WAKUTWA WAMEKUFA KWENYE MSITU MWANZA.

Wanawake watatu ambao hawajatambulika kwa majina, wamekutwa  wamekufa kwenye msitu uliopigwa marufuku kuingia watu uliopo mpakani mwa Mkoa wa Shinyanga na Wilaya ya Misungwi katika Mkoa wa Mwanza.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza Ahmed Msangi, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema kuwa wanawake hao kutoka vijiji tofauti waliingia  ndani ya msitu kwa ajili ya shughuli mbalimbali zikiwemo kusenya kuni na kuchoma mkaa, ambapo walipatwa na mauti.

"Umbali wa kutoka kwenye vijiji vinavyozunguka msitu huo inakadiriwa kuwa wa Kilomita Tano hadi Sita, tuliwakuta wamepatwa na mauti, katika sehemu tofauti katika pori hilo, ambapo mmoja amekutwa amenyongwa huku dalili zikionesha alibakwa, alisema DCP Msangi.

Aidha Kamanda Msangi ameomba wananchi kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi kwa lengo la kuwatambua watu wanaofanya matukio kama hayo, ambapo amesema kuwa amepeleka askari wa kutosha katika eneo  hilo huku akiahidi kuwakamata watu wanaoendesha matukio kama hayo.

Pia Kamanda Msangi amewataka wananchi kutoingia katika msitu huo kama walivyotangaziwa na viongozi wao hapo awali na endapo wanataingia kwa ajili ya shughuli zao waingie wakiwa katika kundi ambapo amebainisha kuwa sehemu hiyo ni hatarishi na kuna wanyama kama nguruwe pori, fisi na viumbe wengine wanapatikana.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.