ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, August 28, 2018

VIDEO:- "VITA DHIDI YA WAHALIFU NI HADI NDANI YA JESHI LA POLISI" - RPC MPYA MWANZA



NA ZEPHANIA MANDIA/GSENGOtV

Kamanda mpya wa Jeshi la Polisi mkoani Mwanza ACP Jonathana Shanna, amezungumza na Maafisa wa Jeshi la Polisi mkoani hapa, ambapo ameonya kuhusu vitendo vya uhalifu na kuahidi kuvitokomeza kwa udi na uvumba.

Kamanda Shanna alifanya mazungumzo na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella baada ya kufika ofisini kwake kujitambulisha.

Naye Mongella alitumia fursa hiyo kuagana na aliyekuwa Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza DCP Ahmed Msangi ambaye amehamishiwa Makao Makuu ya Jeshi hilo jijini Dar es salaam.

Aidha mazungumzo hayo yalijikita zaidi katika kuendelea kuimarisha hali ya ulinzi na usalama mkoani Mwanza, ambapo awali DCP Msangi aliwasihi maafisa hao kumpa ushirikiano wa kutosha kama waliokuwa wakimpa ili kutimiza vyema majukumu yake.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.