ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, August 30, 2018

"SINA BIFU NA MEYA WA JIJI LA MWANZA" ASEMA MKURUGENZI KIOMONI KIBAMBA


GSENGOtV
"Mimi na Meya ni marafiki"
"Ni rafiki yangu, tuko vizuri"
"I wish siku moja tuje naye hapa" 

Ni kauli ya Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Kiomoni Kibamba akijibu swali la mtangazaji wa kipindi cha KAZI NA NGOMA toka Jembe Fm, Mansour Jumanne, wakati akitoa ratiba ya mbio za Mwenge wa Uhuru hii leo, unaotarajiwa kuingia katikati ya Jiji la miamba (Mwanza) Kesho tarehe 1 Mwezi September 2018 kukagua na kuzindua miradi mbalimbali iliyo chini ya mipango ya utekelezaji wa ilani ya CCM kupitia fedha za Serikali.

Ikumbukwe mnamo October 30 mwaka jana 2017 Meya wa Jiji la Mwanza, James Bwire alikamatwa na jeshi la Polisi, na kuswekwa ndani saa chache kabla ya Mhe. Rais John Magufuli kutua jijini hapa kwa ziara, huku kukiwa na sintofahamu ya mahusiano na mvutano kati yake na Kibamba ambaye ni Mkurugenzi wa Jiji, na ikasemekena kuwa Mkurugenzi ni mmoja kati ya watu walioinjinia mpango huo wa kumweka nyuma ya nondo. 

MASWALI MENGINE ALIYOJIBU
- Hana shaka na miradi ya inayokwenda kuzinduliwa/kukaguliwa na Mwenge 2018

- Vipi kuhusu mikopo na taratibu zake jeh anasema nini juu ya shutuma kwamba ipo kwaajili ya kukifeva wadau wa chama tawala pekee?

- Fununu za yeye kuwania nafasi za siasa chaguzi zijazo hususani UBUNGE Jeh ni kweli?

- Kafunguka pia kuhusu kuirudisha hadhi na heshima ya usafi ya Jiji la Mwanza kitaifa na Kanda ya Afrika Mashariki.

- Mkurugenzi wa Jiji ndiye Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi ya Wilaya, Jeh unaweza kuwatangaza wapinzani kuwa ni washindi pindi pale watakaposhinda?

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.