ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, August 31, 2018

MWENGE WA UHURU WATINGA JIJINI MWANZA.

NA ZEPHANIA MANDIA/GSENGOtV
PICHANI JUU:- Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza Mhe. Dkt. Philis Nyimbi akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkuu wa Wilaya Sengerema Mhe. Mwl. Emmanuel Kipole baada ya kumaliza mbio zake wilayani Sengerema na Buchosa.
Miradi itakayopitiwa na mbio za Mwenge kwa Halmashauri ya jiji la Mwanza ina thamani ya shilingi bilioni 4.8.
Katika eneo la Kamanga Feri jijini hapa, mapokezi yamefanyika mapema leo asubuhi ambapo Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa Injinia Charles Francis Kabeho ametumia fursa hiyo kuwahimiza wazazi na walezi kutimiza wajibu wao kwa kuwapa mahitaji muhimu ya shule watoto wao katika kipindi hiki ambacho serikali inatekeleza mpango wa elimu bure ili kuwawezesha kupata elimu bora.

Aidha ameonya kuhusu suala la dawa za kulevya kwa vijana ambapo amewataka kujiepusha na matumizi ya dawa za kulevya kwa kuwa yanahatarisha maendeleo ya taifa na kuwahimiza kuwa wazalendo.
Hatua kwa hatua za makabidhiano.

Mwenge wa Uhuru mikononi mwa Mbunge wa jimbo la Nyamagana Stanslaus Mabula.

Mwenge wa Uhuru mikononi mwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya jiji la Mwanza Mhe. Kiomoni Kibamba.




Ngoma asili.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.